Jumapili, 21 Januari 2018

JIFUNZE KUSINDIKA NYANYA

                              KUSINDIKA NYANYA
Nyanya ni zao ambalo haliwezi kuifadhika kwa muda mrefu lisipozindikwa zao hili ni zao la bustani ambalo linalimwa na wakulima na linahitajika katika shughuli za jikoni kama kiungo cha kuungi  mboga, wakulima wemgi wamekuwa wakipata hasara kwa kulima zao la nyanya na kukata tamaa ya kulima zao hili tena ni kwanini kwa sababu bei ya zao hushuka pale ambapo zao hilo linapatikana kwa wingi sokoni na kumfanya mkulima ashidwe kupata faida kwa sababu zao linapokuwa lipo kwa wingi sokoni na uhitaji wa watu ni mdogo bei hushuka lakini kunakipindi ambacho zao halipatikani kwa wingi sokoni na kuwa na bei kubwa kipindi hiki ni kipindi ambacho mkulima ambaye ni mbunifu anatengeneza pesa lakini atatengenezaje pesa ni kwa kuchakata zao hilo na kulihifadhi na kuuzwa kwa bei ya juu.
Zao la nyanya ni zao ambalo hisindikwa na kupata bidhaa mbalimbali kuepuka uhalibifu wa zao hilo, kuongeza ubora na thamani, na kuwezesha upatikanaji wakati wote, zao hili huzidhikwa kuwa nyanya za kukausha,juice,lahamu na sosi au rojo.

KUKAUSHA NYANYA
Nyanya zinazotakiwa ni zile zilizokomaa na kuiva vizuri. Aina ya nyanya zinazotakiwa ni zile zenye nyama nyingi kama roma, Tanya na tengeru 97.

Vifaa
Visu vikali visivyoshika kutu
Ungo
Sufuria
Jiko
Kaushio bora
Mifuko ya plastiki
Beseni
Jinsi ya kukausha
chagua nyanya zilizokomaa na kuiva vizuri
osha kwa maji safi na salama
kata nyanya kwenye vipande visivyozidi muilimita tano
panga kwenye kaushio safi ili zikauke
fungasha vipande vya nyanya vilivyokauka kwenye mifuko safi ya plastiki isiyopitisha unyevu
weaka lebo inayoonyesha muda wa kuisha matumizi kwa mwaka mmoja kutoka siku  ya kutengenezwa
hifadhi sehemu yenye ubaridi na kavu.
Hutumika kama viungo kwenye vyakula mbalimbali

KUSINDIKA NYANYA KUPATA JUISI
chukua nyanya zilizoiva na kukomaa vizuri
osha kwa maji safi na salama
katakata nyanya katika vipande vidogo
pima uzito wa nyanya
kwa kilomoja ya nyanya ongeza maji lita moja
chemsha kwemye moto kwa muda wa dakika 5 moto uwe na nyuzi joto 85
saga nyanya kwa kutumia mashine ya mkono au umeme
chuja rojo ili kupata juisi
ongeza sukari gram 20 na chumvi gram 10 kwa kila lita moja ya rojo
chemsha tena kwa muda wa dakika 20
jaza juisi ikiwa ya moto kwenye chupa safi
zipange chupa hizo kwenye sufuria
weka maji kwenye sufuria yafii nusu ya chupa
chemsha tena ili kuondoa hewa iliyoupo ndani ya chuapa
ipua acha zipoe kisha weka lebo
ifadhi kwenye ubaridi
juisi hii huifadhiwa kwa muda wa miezi sita
hutumika kama kiburudisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

UFUGAJI WA KUKU KIBIASHARA

JIFUNZE KUFUGA KIBIASHARA HASA KWA WAFUGAJI WA KUKU KWA YOYOTE ATAKAYE HITAJI TEMPLATE HII NA ZINGINE ANITAFUTE KWENYE NO 0756841313