SABABU ZA KUKU KUTOTAGA
Kuku hupunguza utagaji na hata kuacha kutaga kabisa iwapo:-
Hawakupewa chakula bora au cha kutosha.
Hawapewi maji safi ya kutosha.
Wamebanana, yaan hawakai kwa raha.
Vyombo vya maji au chakula havitoshi.
Mwanga hautoshi.
Majogoo yamezidi (weka jogoo 1 kwa mitetea 10)
Kuku wanaumwa.
Wana vidusa vya nje na ndani (external and internal parasite).
Wamezeeka (umri zaidi ya miaka miwili na nusu).
Maumbile ya kuku mwenyewe.
NINI KIFANYIKE
Wape kuku chakula bora na cha kutosha (gram 110 - 120 kwa kuku kwa siku).
Wape maji safi ya kutosha, wanywe maji saa moja zaidi baada ya kuwalisha
chakula.
Weka idadi ya kuku inayolingana na nafasi iliyopo. Weka kuku 3 - 4 kwa
meta moja mraba.
Weka vyombo visafi na vya kutosha.
Hakikisha chumba kina mwanga wa kutosha. Mwanga unaowatosha kuku ni
ule unaoruhusu mtu kusoma gazeti.
Weka idadi ya vyombo kulingana na mitetea iliyopo. Jogoo 1 kwa mitetea 7 -
10.
Watenge na kutibu kuku wagonjwa. Na wachanje kuku ukifuata kalenda.
Tibu vidusa vya ndani na nje (external and internal parasite) kwa kufuata
ratiba au kila unapoona dalili.
Ondoa kuku wazee kwa kuuza au kuchinja.
Ondoa kuku wasio taga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni