Jumapili, 24 Juni 2018

Maajabu ya mkojo wa sungura

MAAJABU YA MKOJO WA SUNGURA

Licha ya kuwa wafugaji wengi wamekuwa wakifuga kwaajili ya nyama, zao la Mkojo wa Sungura kwa faida yake pengine ndo kubwa kuliko mazao mengine yote

MATUMIZI YA MKOJO WA SUNGURA

Kutokana na kuwa na kiwango kik cha madinitrogen phosphorus na potassium mbolea ya Mkojo wa Sungura imekua mbadala wa mbolea za NPK na CAN ambazo kwa kiasi kikubwa zimekua zikichangia ongezeko la soil acidity Ikitumika katika ratio ya lita moja ya Mkojo wa Sungura kwa lita 5 za maji kunyunyuzia katika majani au ardhi wakati wa asubui au jioni kipindi ambapo stomata zipo wazi itakupa matokeo mazuri katika viazi,maharage,miche ya matunda, mbogamboga, mahindi na mazao mengine

Lakini pia Kama kimiminika cha asili chenye uwezo wa kurudisha rutuba iliyopotea ardhini Matumizi ya Mkojo wa Sungura Kama kiuatirifu (insecticides) Mkojo wa Sungura una,kiasi kikubwa cha Ammonia ambayo ndio makali yake halisi ambayo Uharibu kabisa mazingira rafiki ya uzalianaji wa bacteria na fangasi katika mmea Mkojo wa Sungura ukitumika kwa kiasi cha lita 1 katika Lita 2 hadi 3 za maji kunyunyuzia katika majani ambayo yameshambuliwa na wadudu kila siku,huua wadudu na kurejesha afya ya mmea Mkojo wa Sungura huua wadudu kama aphids,fungus, mites ,leaf miners nk

Katika mmea ambao haujashambuliwa, ukinyunyuzia kwa wiki Mara,moja inatosha kuupatia mmea afya bora,ustahimilivu wa magonjwa ya bacteria na fangasi pia kukupatia mavuno mengi
Mbolea ya mkojo wa sungura ni mbolea bora zaidi yenye kuleta faida kubwa kwenye udongo kwani ina uwezo wa kufufua ardhi iliyokufa ambayo ilikua haifai kwa matumizi ya kilimo pia huleta faida kwa mkulima kwa kuongeza kipato kwa ongezeko la uzalishaji shambani kwake.

Mbolea hii ina virutubisho vingi ndani yake ikiwemo nitrogen, phosphorus, pottasium na virutubisho vingine vidogo vidogo ( micro nutrients) kama vile calcium, magnesium, boron, zinc, manganese, sulfur,copper, cobart na vingine vingi ikiwemo na wadudu wadogo wadogo wanaohitajika katika udongo ( micro organisim)

Angalizo;-
Usitumie Mkojo wa Sungura ambao haujachanganywa na maji.

Alhamisi, 7 Juni 2018

USINDIKAJI WA MAPAPAI NA MAPARACHICHI


Kusindika Mapapai
Mapapai husindikwa kupata bidhaa kama juisi, jamu na matunda makavu.
 Kusindika mapapai kupata juisi
Vifaa
• Visu vikali visivyoshika kutu
• Vyombo vya kuoshea matunda
• Mashine ya kusaga matunda
• Kipimo cha sukari (Refractometer)
• Chupa zenye mifuniko imara
• Saa
• Lebo na lakiri
• Kipima joto
• Sufuria
• Jiko
• Mwiko
• Vitambaa au chujio safi
Mali ghafi ya kutengeneza lita tatu za juisi.
• Mapapai mawili ya ukubwa wa kati
• Sukari gramu 100
• Juisi ya malimau kikombe cha chai kimoja
• Maji safi lita tatu
Jinsi ya kusindika
• Osha matunda kwa maji safi na salama
• Menya kuondoa maganda na mbegu
• Kata katika vipande, kisha saga kwa kutumia mashine kupata rojo.
• Ongeza maji ya ndimu au malimau kupata ladha. Katika kila lita moja ya rojo ya mapapai
weka kikombe kimoja cha chai cha juisi ya ndimu au malimau ili kuongeza ladha na kuboresha
uhifadhi. Ongeza maji safi kiasi cha lita tatu.
• Chuja kwa kutumia chujio safi
• Chemsha mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 20 ukiwa unakoroga katika joto la nyuzi
80 hadi 90 za Sentigredi.
• Ipua
• W eka juisi kwenye chupa safi zilizochemshwa ikiwa ya moto kisha funga kwa mifuniko
imara.
• Panga chupa kwenye sufuria kisha weka maji kufikia nusu ya kimo cha chupa.
• Chemsha chupa kwa muda wa dakika 20 ili kufisha bakteria na vimelea vingine.
• Ipua chupa na acha zipoe
• W eka lebo
• H ifadhi katika sehemu safi yenye hali ya joto lisilozidi nyuzi 25 za Sentigredi na isiyo na
mwanga mkali.
Matumizi
Juisi hutumika kama kinywaji au kiburudisho na ina virutubishi vya vitamini C, na A kwa wingi.
Kusindika mapapai kwa kukausha
Vifaa
• Kaushio bora
• Mashine ya kufungia au mishumaa ama jiko la mkaa
• Meza ya kukatia
• Kisu kisichoshika kutu
• Beseni la kuoshea
• Mifuko ya plastiki au chupa za plastiki au kioo
Malighafi/Mahitaji
• Mapapai yaliyonza kuiva
• Maji ya malimau au ndimu
Jinsi ya kutengeneza
• Osha mapapai yaliyoiva vizuri na yasiyo na magonjwa wala mikwaruzo.
• Menya kwa kutumia kisu kikali kisichoshika kutu
• Kata katika vipande visivyozidi urefu wa sentimita kumi na unene wa milimita tatu. Ukizidisha
ukubwa vipande havikauki vizuri na ubora wake hushuka.
• Viweke vipande hivyo ndani ya maji ya malimao/ndimu kwa muda wa dakika moja hadi mbili
ili kudumisha rangi ya papai na kuongeza ladha.
• Panga vipande kwenye trei za kaushio
• Kausha kwa muda wa siku tatu hadi nne kutegemea hali ya jua.
• Fungasha kwenye mifuko ya plastiki au chupa za kioo safi na hifadhi kwenye sehemu kavu,
yenye mwanga hafifu na safi.
Matumizi ya mapapai
Papai lililoiva
• Huliwa kama tunda
• Hutengenezwa jamu na juisi
• Hukaushwa na kuliwa kwa kuchanganywa kwenye saladi ya matunda au keki
• Hutia ladha kwenye aisi krimu
Papai bichi
Utomvu wa papai bichi hutumika katika matumizi yafuatayo:-
• Kutengeneza peremende, dalia, urembo na madawa ya kulainisha tumbo
• Huwekwa kwenye nguo wakati wa kutengenezwa ili isifupike.
• Hulainisha nyama
• Hulainisha ngozi
Papai bichi pia hutengenezwa:
• Mboga
• Achali.

Kusindika Maparachichi
Kusindika maparachichi kupata guakamole
Vifaa
• Mashine ya kusaga rojo
• Bakuli ya kuoshea maparachichi
• Kisu kikali kisichoshika kutu.
• Chupa za kufungashia zenye mifuniko imara
• Lebo
Malighafi
• Maparachichi mawili
• Kitunguu maji kimoja
• Pilipili kali moja
• Juisi ya limao kidogo
• Giligilani ya majani 25
• Chumvi na pilipili manga kidogo.
• Maji safi na salama.
• Nyanya moja kubwa.
Jinsi ya kutengeneza
• Menya kitunguu
• Kata kitunguu na pilipili kali
• Osha maparachichi na giligilani
• Saga gilgilani kwenye mashine ya kusaga
• Ongeza maparachichi, juisi ya limao, nyanya, pilipili, kitunguumaji. Chumvi na pilipili manga.
• Saga hadi mchanganyiko uwiane.
• Fungasha guakamole kwenye chupa za kioo
• W eka lebo
• Hifadhi mahali peny baridi.
Matumizi
Hutumika kama sosi baridi pamoja na vitafunwa kam mikate au pamo

UFUGAJI WA KUKU KIBIASHARA

JIFUNZE KUFUGA KIBIASHARA HASA KWA WAFUGAJI WA KUKU KWA YOYOTE ATAKAYE HITAJI TEMPLATE HII NA ZINGINE ANITAFUTE KWENYE NO 0756841313